Pata Habu kwa urahisi kwenye simu yako:
Unaweza kuongeza njia ya mkato ya kuingia katika tovuti yoyote kwenye Skrini ya kwanza ya simu yako. Hii hukusaidia kuifungua haraka, kama vile kufungua programu. Mchakato wa kuongeza tovuti kwenye skrini yako ya kwanza ni rahisi na huchukua chini ya dakika moja. Hivi ndivyo unavyoweza kufanya kwa ajili ya Hub:
iPhone
1. Ingia kwenye Programu tumizi ya Safari kwenye simu yako ya iPhone.

2. Ingia kwenye tovuti unayotaka kuongeza kwenye skrini yako ya kwanza ya (https://deafblindness.info/)

3.Chagua kitufe cha Shirikisha/Zaidi katika upau wa vidhibiti wa Safari

4. Shusha chini orodha ya machaguo, kisha Shuka chini kisha ubofye neno Ongeza kwenye Skrini ya kwanza (huenda ikakubidi kubofya kwenye neno Zaidi ili uweze kuona chaguo).
Ikiwa huoni neno Ongeza kwenye Skrini ya kwanza, unaweza kuiongeza. Sogeza chini orodha ya machaguo, bofya neno Badilisha Vitendo, kisha ubofye neno Ongeza kwenye Skrini ya kwanza.

5. Ipe jina kisha bofya neno ‘Ongeza’

Android
- Kwenye kifaa chako cha Android, fungua Kivinjari cha Chrome.

2. Nenda kwenye tovuti unayotaka kutengeneza njia ya mkato.

3. Upande wa kulia wa upau wa anwani (nukta tatu), bofya neno Zaidi kisha Ongeza kwenye skrini ya kwanza na tengeneza njia ya mkato.

- Kutoka kwenye kidirisha kinachoonekana:
• Badilisha jina: Chagua jina chaguo-msingi la njia ya mkato au ubadilishe njia ya mkato.
• Inaweza pia kukupa chaguo la kubinafsisha aikoni

5. Gonga Ongeza.
