Mwaka wa kuchapishwa
February 2025

Tazama rasilimali na taarifa za serikali za mitaa, mashirika yasiyo ya kiserikali na mashirika ya kimataifa yasiyo ya kiserikali ili zikusaidie kupitia maisha ya kila siku.

Ulemavu: IN

Ulemavu :IN inatoa taarifa kuhusu sheria, mahitaji ya ajira, mahitaji ya ufikiaji na umaizi wa data.

Tanzania Health Promotion Support (THPS)

THPS inatoa taarifa kuhusu huduma za afya na mipango ya kukuza afya nchini Tanzania.

Jarida la taarifa za Afya Tanzania

Jarida la Taarifa za Afya Tanzania linatoa taarifa kuhusu data za takwimu, ripoti, na kuhusu viashirio na mienendo ya afya nchini Tanzania.

Tanzania Association of the Deafblind (TADB)

TADB ni shirika lisilo la faida linalofanya kazi kuboresha maisha ya viziwi kupitia uhamasishaji, ushiriki na elimu. Pia wana jukwaa la lugha ya ishara ili kusaidia katika mawasiliano.

Kyaro Assistive Tech

Kyaro Assistive Tech ni shirika lisilo la kiserikali lililosajiliwa nchini Tanzania linalounda na kusambaza vifaa saidizi.

Maelezo ya Ufikiaji wa Tovuti 

Katika baadhi ya maeneo kwenye tovuti yetu, tunashiria au kukuelekeza katika tovuti za watu wengine na programu ambazo hutoa taarifa muhimu na ushauri kwa watumiaji wetu. Hta hivyo, hatuwezi kuthibitisha kwamba tovuti na programu hizi za washirika wengine zinapatikana kikamilifu na zinatii miongozo ya WCAG 2.2.

Pale inapowezekana tunajitahidi kushirikiana na wahusika hawa kufanya mabadiliko yanayohitajika ili kuendana na miongozo ya WCAG2.2 na kuboresha ufikiaji wao.

Je, hii ilifaa

Changia


Raslimali zinazofanana

Utangulizi wa Sense International Tanzania na Uziwikutoona

Rasilimali hii inahusu upimaji na utambuzi wa awali wa watoto wenye ulemavu wa uziwikutoona (yaani, matatizo ya kusikia na kuona kwa pamoja) ili kuhakikisha wanapata msaada unaofaa wa kitabibu, kielimu, na katika kujifunza stadi za maisha kupitia ushirikiano kati ya wataalamu wa afya na walezi.

Muhtasari wa Sera ya Elimu na Mafunzo, Toleo la 2023

Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2023 ni mfumo wa kina unaoongoza maendeleo ya mfumo wa elimu jumuishi, wa haki na wenye ubora nchini Tanzania, kwa kuweka mkazo kwenye upatikanaji, umuhimu wa maudhui, na ujifunzaji wa maisha yote kwa wote, wakiwemo makundi yaliyo maalum.

Muhtasari wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, 2010 

Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya mwaka 2010 ni sheria iliyotungwa kulinda haki na kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu nchini. Inahakikisha wanatendewa kwa haki, wanapata fursa sawa, na wanaweza kushiriki kikamilifu katika jamii kama watu wengine. Muhtasari huu unaelezea kila sehemu ya Sheria ili kuwasaidia wasomaji kuelewa madhumuni yake…