Je, hii inamfaa nani?

Utambuzi na tathimini ya mapema, wazazi, waangalizi

Mwaka wa kuchapishwa
June 2025
Imetengenezwa na
Sense International Tanzania

Rasilimali hii inatoa maelezo kuhusu upimaji na utambuzi wa awali wa watoto wenye ulemavu wa uziwikutoona, ikieleza hatua za mchakato huo, huduma zinazopatikana, na jukumu la wahudumu wa afya pamoja na walezi katika kuhakikisha watoto wanaopatikana na hali hiyo wanapata msaada wa bure, wa kitabibu na kielimu unaoendana na mahitaji yao.

Sisi ni nani?

Sense International ni shirika la kimataifa linalotoa huduma kwa watu wenye ulemavu wa Uziwikutoona na wale wenye ulemavu mchanganyiko unaopelekea milango mingine ya fahamu (kuona, kusikia, kugusa na kuonja) kushindwa kufanya kazi vizuri.

Tunafanya nini?

Tunashirikiana na serikali pamoja na mashirika mbalimbali katika kuwatambua watu wenye Uziwikutoona na wale wenye ulemavu mchanganyiko ili kuwawezesha kiafya, kielimu na kujifunza stadi za maisha.

Itakuwaje kama mtoto wangu akigunduliwa kuwa na ulemavu wa Uziwikutoona?

Mtoto akigunduliwa kuwa na ulemavu wa Uziwikutoona au changamoto kwenye utendaji wa milango ya fahumu (kuona na kusikia) ataandikishwa katika kituo cha kutolea huduma ili aweze kusaidiwa na wataalamu wa tiba kwa vitendo. Wataalamu hao wataandaa utaratibu maalumu kwa kila mtoto ili kumsaidia, na kuwafundisha wazazi au walezi namna ya kusawasaidia watoto wao wakiwa nyumbani. Pia watawatembelea wanakoishi ili kujua maendeleo yao.

Tunafanyaje?

Hatua ya kwanza: Watoto wenye umri wa siku moja hadi miaka mitano watabainiwa kama wana viashiria vya kuwa na ulemavu wa uziwikutoona. Zoezi hili litafanywa na wahudumu wa afya kwa ngazi ya jamii wawapo katika vituo vya chanjo au sehemu tofauti tofauti ndani ya kata husika.

Hatua ya pili: Kama mtoto atakuwa na viashiria vya Uziwikutoona ataelekezwa kwenda kufanyiwa vipimo zaidi kwa kutumia vifaa maalumu katika moja ya vituo vifuatavyo vya afya vinavyomilikiwa na serikali, Mbagala Round Table, Yombo Vituka, Mbande, Hospitali ya Rufaa Temeke.

Ni muda gani muafaka kumpima mtoto wangu?

Kwa matokeo mazuri mtoto anatakiwa kupimwa kati ya masaa 24 baada ya kuzaliwa hadi umri wa miaka mitano.

Vipi kama mtoot wangu atakuwa na ulemavu wa aina moja tu?

Iwapo mtoto atagunduliwa kuwa na changamoto katika mlango mmoja wa fahamu (masikio au macho) ataelekezwa kuwaona wataalamu katika Hospitali ya Rufaa ya Temeke watakaoweza kumsaidia kupata msaada wa kitabibu kwa utaratibu uliopo.

Je, natakiwa kulipia gharama yoyote?

Hapana, huduma hii inatolewa bure bila malipo yoyote.

Je, hii ilifaa

Changia


Raslimali zinazofanana

Muhtasari wa Sera ya Elimu na Mafunzo, Toleo la 2023

Sera ya Elimu na Mafunzo ya mwaka 2023 ni mfumo wa kina unaoongoza maendeleo ya mfumo wa elimu jumuishi, wa haki na wenye ubora nchini Tanzania, kwa kuweka mkazo kwenye upatikanaji, umuhimu wa maudhui, na ujifunzaji wa maisha yote kwa wote, wakiwemo makundi yaliyo maalum.

Muhtasari wa Sheria ya Watu Wenye Ulemavu, 2010 

Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya mwaka 2010 ni sheria iliyotungwa kulinda haki na kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu nchini. Inahakikisha wanatendewa kwa haki, wanapata fursa sawa, na wanaweza kushiriki kikamilifu katika jamii kama watu wengine. Muhtasari huu unaelezea kila sehemu ya Sheria ili kuwasaidia wasomaji kuelewa madhumuni yake…

Muongozo wa mwalimu wa kumfundisha mwanafunzi mwenye uziwikutoona katika elimu ya awali na msingi darasa la I-II

Mwongozo wa mwalimu unaotoa mikakati na msaada wa kuwafundisha kwa ufanisi wanafunzi wenye ulemavu wa kusikia au kuona katika shule za msingi za awali ili kuendeleza elimu jumuishi.