Nchini Tanzania, inakadiriwa kuwa takribani watu milioni 1.16 wanaishi na aina ya uziwikutoona mdogo na zaidi ya watu 115,000 wanaishi na aina ya Uziwikutokuona mkali zaidi.*
*Shirikisho la uziwikutoona Duniani, 2018 Katika hatari ya kutengwa kwenye utekelezaji wa CRPD na SDGs: Kutokuwepo kwa usawa kwa watu wenye uziwikutoona.
Watu wenye ulemavu ni miongoni mwa makundi maskini na yaliyotengwa zaidi nchini Tanzania. Bado hakuna utambuzi wa ulemavu wa uziwikutoona kama ulemavu unaojitosheleza na hivyo, inafanya kuwa vigumu kupata huduma na usaidizi kwa ajili ya mahitaji yao maalum.
Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya mwaka 2010 inatoa huduma za afya, msaada wa kijamii, upatikanaji, ukarabati, elimu na mafunzo ya ufundi stadi, mawasiliano, ulinzi wa ajira au kazi na uendelezaji wa haki za msingi kwa watu wenye ulemavu na kutoa masuala yanayohusiana nayo.
Watu wenye, uziwikutoona bila kujali asili ya ulemavu wao, hupata ugumu wa kupata taarifa muhimu, habari, mawasiliano, michezo, utendaji kazi wa maisha ya kila siku, na mwingiliano wa kijamii. Ingawa uzoefu huu unatofautiana kati ya watu walio na hali ya kuzaliwa nayo dhidi ya ile inayopatikana baada ya kuzaliwa, kwa ujumla wote wanapata changamoto zinazofanana pamoja na ufikiaji wa msaada binafsi wanaohitaji.
Ufikiaji wa teknolojia unaweza kuwa chanzo cha mabadiliko kwa watu wenye ,uziwikutoona kutoa njia mpya za kupata habari, kuwasiliana na watu wengine, na kushiriki kikamilifu katika maisha ya kila siku.
Raslimali hizi zitawawezesha watu wenye uziwikutoona na wale wanaowasaidia kuishi, kujifunza, na kustawi.
Uziwikutoona ni nini
Ukurasa huu unakueleza uziwikutoona ni nini. Pia unashughulikia aina tofauti za ,uziwikutoona sababu zake kwa watoto wachanga na watu wazima, utambuzi, viashiria vya Uziwiupofu, kutibu visababisi vya msingi na kudhibiti hali hiyo.
Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu wenye Ulemavu
Huu ni uwasilishaji mfupi wa baadhi ya haki za watu wenye ulemavu, kama zinavyofafanuliwa katika vifungu vya Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu wenye Ulemavu. Hii sio hati ya kisheria.
Jinsi ya kumsaidia mtoto mwenye uziwikutoona katika miaka yake ya awali
Miaka ya awali ya maisha ya mtoto inaweza kuwa mkondo wa kujifunza kwa wazazi. Katika ukurasa huu utaweza kutapata majibu ya baadhi ya maswali ya kawaida zaidi ambayo huulizwa na wazazi na walezi wa watoto wadogo wenye ulemavu changamano.