Je, hii inamfaa nani?

• Wanafunzi
• Wazazi
• Watunga sera

Mwaka wa kuchapishwa
May 2026
Imetengenezwa na
Sense International Tanzania

Maudhui haya yanaelezea namna ya kumfundisha mwanafunzi mwenye uziwikutoona.

Manuscripti ya video

Madam Maula amekaa darasani, baadhi ya vifaa vya kufundishia kama ubao vinaonekana nyuma yake.

Madam Maula

Mahitaji ambayo mwalimu anatakiwa ayafahamu kabla hajaanza kumfundisha mtoto. Kwanza afahamu huyo mtoto ana matatizo gani kutoka na IP aliyoitengeneza. Atengeneze IP ili kujua mtoto anaweza nini? Anashindwa nini kukifanya? Anaulemavu gani?

Katuni ya mwalimu akiingia darasani huku wanafunzi wakionekana wenye furaha kumuona.

Madam Maula

Katika kuona, kusikia au ana ulemavu mwingine, pale ndio utaamua uanze unafundisha nini utaangalia na akili ilivyo. Hapo nido utaanza.

Mahitaji, yanategemea mtoto na uhitaji wake ulivyo. Kiziwi asiyeona labda kiziwi ambaye haoni kabisa hasikii kabisi lakini akili yake iko safi. Huyo tutatumia lugha alama mguso.

Katuni ya mwalimu anamsogelea mwanafunzi mwenye uziwikutoona kisha anawasiliana nae kwa lugha ya alama.

Madam Maula

Kwa sababu akili iko safi, unaweza kumfundisha kitu chochote. Unaanzia pale vitu ambavyo yeye anaweza kuvifanya, unaviboresha. Halfu ndio unaingia kwenye vitu ambavyo unataka wewe umfundishe. Kwa mfano, mtoto alikuwa anakula kwa mkono….

Wanafunzi wawili wamekaa darasani peke yao, kamera inawasogelea kwa karibu wakiwa wanakula chakula kwa kutumia vijiko.

Madam Maula

…amezoea, msadie aweze hata kutumia kijiko ili aweze kula, mtoto alikuwa anakaa chini anapokula, muweke katika kiti, muweke mezani, aweze kutumia meza kwa kula. Unakuwa unaboresha ule uelewaji wake kutoka anachoweza kwenda asichoweza. Na pia kutoka vitu vidogo vidogo kwenda vitu vikubwa. Huwezi kuanza vitu vidogo kwenda vikubwa hata elewa.

Hata vifaa vinategemea, kwa mfano kiziwi asiyeoona ambaye hana baki ya usikivu wala baki ya uoni huyu tunatumia vifaa vya kugusa zaidi. Vifaa vya kugusa zaidi inabidi mwalimu uviandae, akishagusa, utafute pia vifaa ambavyo ni halisi. Kwa hiyo atalinganisha vile vya kugusa atagusa na kifaa halisi. Kwa hiyo ataelewa alikuwa anataka nini.

Kwa mfano nataka nifundishe matunda, mtoto ajue matunda. Nitachukua chungwa nitalichora, nitaweka alama za kugusa, atagusa atajua hili ni chungwa. Halafu sasa nachukua chungwa halisi ninampa ili aelewe zaidi nitalimenya lile chungwa na kulikata na kula hapo utakuwa umemuhisha kwamba, lile nililogusa ni sawa sawa na tunda halisi, na tunda hilo likoje? Liko hivi lina utamu hivi. Kwa hiyo ukimpa kitu kingine atatofautisha chungwa na ndimu  pamoja kama zinafanana kwa sababu ameshazionja  umbo ni lilelile. Ukichukua ndimu kubwa na chungwa kubwa ukampa atatofautisha kwa sababu ataangalia, atagusa umbo lilivyo. Pia wakati ukilikata ataona chungwa ni tamu kuliko ndimu au limao ulilompa ashike. Kwa hiyo mtoto atakuwa ameshahuhisha maarifa kwa hiyo kumfundisha mtoto, mahitaji ya mtoto yanategemea ulemavu wake ulivyo ndio utajua mwalimu nifanye nini ili mtoto aweze kupata elimu.

Je, hii ilifaa

Maelezo haya yamekusaidia?

Changia


Raslimali zinazofanana

Darasa la mwanafunzi mwenye uziwikutoona

Video ya mwalimu wa kitengo maalumu akielezea namna ya kuliweka darasa la wanafunzi wenye uziwikutoona.

Mchezo Wa Mjongeo Na Hisia Kwa Watoto Wenye Uziwikutoona: Seti Ya Zana Kwa Mtoa Huduma

Rasilimali hii inatoa mwongozo hatua kwa hatua kuhusu kutumia michezo na shughuli za mwendo—kama vile kuzungusha, bakuli za hisia, na michezo ya mpira—kusaidia maendeleo ya mwili, hisia, na kijamii kwa watoto wenye ulemavu wa kusikia na kuona.

Marekebisho ya Darasa kwa Ajili ya Wanafunzi Wenye Uziwikutoona

Rasilimali hii inatoa mwongozo juu ya jinsi ya kufanya marekebisho ya darasani kwa watoto wenye ukosefu wa macho na kusikia.